Tufanye toba ya kweli kupata amani - Dkt. Biteko

 

Baada ya Hekaheka za wiki nzima, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko amewasihi watanzania kufanya toba ya kweli kupata amani.

Dkt. Biteko ameyasema hayo wakati alipoungana na Wana Bukombe pamoja na wakazi wa maeneo jirani kumuabudu Mwenyezi Mungu kupitia Mkesha wa “Ibada Halisi Bukombe Night of Worship” uliofanyika Septemba 20, 2025 katika Uwanja wa Shule ya Msingi Igulwa, Bukombe.

“Uzima tulionao leo ni Wimbo mpya kinywani mwetu, Afya tulionayo ni Wimbo mpya kinywani mwetu, Hata Bukombe vile tulivyo ni wimbo mpya kinywani mwetu”.

Ibada hiyo iliyoandaliwa kwa pamoja na Ibada Halisi Team na kanisa AICT Ushirombo imehudhuriwa na waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili akiwemo Ambwene Mwasongwe, Rehema Simfukwe, Jonathan Kartagata, Joshua Lugendo na Agape Gospel Band.



Chapisha Maoni

0 Maoni