Mchezaji
nyota wa tenisi kutoka Marekani, Taylor Townsend, ameomba radhi kufuatia kauli
zake za kuviponda vyakula vya jadi vya Kichina alizotoa kupitia mitandao ya
kijamii, ambazo zimeibua mjadala mkali.
Townsend
(29), ambaye kwa sasa yuko katika jiji la Shenzhen nchini China kwa ajili ya
mashindano ya Billie Jean King Cup Finals, alichapisha video kupitia Instagram
akizungumzia baadhi ya vyakula alivyovikuta, ikiwemo vyenye vyura, kasa na
tango bahari, akisema:
“Hii ni
kitu cha ajabu kabisa kuwahi kuona... Inabidi niongee na HR... kula kasa na
vyura ni kitu cha mwituni sana.”
Kauli
hiyo ilisababisha mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii, si tu kwa
Kiingereza bali pia kwenye majukwaa ya Kichina, ambako wengi walieleza
kuchukizwa na namna alivyodhalilisha utamaduni wa chakula wa China.
Baadaye,
Townsend ambaye kwa sasa ndiye mchezaji namba moja kwa ubora duniani upande wa
mchezo wa ‘doubles’, aliomba radhi akisema:
“Hakuna
kisingizio, sina maneno… kwangu mimi, nitajirekebisha na kuwa bora zaidi.”
Kauli
hiyo imepokelewa kwa hisia tofauti, huku wengi wakisisitiza umuhimu wa
kuheshimu tamaduni za wenyeji, hasa kwa watu maarufu wanaotembelea mataifa ya
wengine.

0 Maoni