Ngorongoro yatinga Ulaya kutangaza utalii na uwekezaji

 

Naibu Kamishna wa Uhifadhi, Huduma za Shirika la Hifadhi ya Ngorongoro, Bw. Aidan Makalla ameongoza ujumbe wa shirika hilo kushiriki katika maonesho ya “My Tanzania Roadshow 2025 Europe”, yenye lengo la kunadi fursa za utalii na uwekezaji katika hifadhi hiyo maarufu duniani.

Bw. Makalla ameambatana na Afisa Utalii Mkuu Msaidizi, Bw. Abdiel Laizer, ambapo wameshiriki kwenye mikutano na majadiliano na mawakala mbalimbali wa utalii kutoka barani Ulaya katika miji ya Stuttgart (Ujerumani), Salzburg (Austria), Ljubljana (Slovenia) na Milan (Italia) kuanzia Septemba 22 hadi 27, 2025.

Maonesho hayo yaliyoandaliwa na Kampuni ya KILIFAIR, yanatajwa kuwa miongoni mwa majukwaa ya kipekee ya kutangaza vivutio vya utalii wa Tanzania, yakilenga kuitangaza nchi kama kitovu cha utalii barani Ulaya.

Takriban kampuni 80 kutoka Tanzania na Ujerumani zinashiriki katika maonesho hayo, zikiwemo kampuni binafsi, taasisi za kiserikali na mashirika ya kimataifa ya utalii.

Maonesho ya "My Tanzania Roadshow" yanatarajiwa kusaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza mwamko wa watalii kutoka bara la Ulaya kuitembelea Tanzania, hususan Hifadhi ya Ngorongoro, Serengeti, Ziwa Natron na maeneo mengine yenye vivutio vya kipekee.



Chapisha Maoni

0 Maoni