NCAA yaadhimisha Siku ya Faru Duniani Karatu

 

Katika kuadhimisha Siku ya Faru Duniani, wananchi wa mji wa Karatu wameungana na Maafisa wa Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Askari wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Karatu, pamoja na wadau mbalimbali wa uhifadhi na utalii kushiriki mbio maalum za kilomita tano zenye lengo la kuhamasisha juhudi za uhifadhi wa mnyama Faru.

Maadhimisho hayo, yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali, yamefanyika leo Septemba 22, 2025  huku yakiongozwa na kaulimbiu isemayo: “Tuhakikishe aina tano za Faru waliopo duniani wanaishi.”

Katika maadhimisho ya Siku ya Faru Duniani Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inafanya shughuli mbalimbali ikiwepo kutoa elimu ya uhifadhi wa Faru kwa jamii, kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira, maonesho ya uhifadhi wa Faru pamoja na Michezo mbalimbali yenye lengo la kuhamasisha uhifadhi wa Faru.







Chapisha Maoni

0 Maoni