Mradi wa Barabara inayowaunganisha wananchi wa kata ya
Katerelo na Kata za Bujugo na
Kasharu Maarufu kama Kyema-Katerelo unaotekelezwa na Wakala ya Barabara za mjini na vijijini (TARURA) kwa kiwango Cha
Lami kilometa 0.55 chini ya mkandarasi wa ndani Kashico LTD umefikia asilimia 80.
Meneja wa TARURA wilaya ya Bukoba Mhandisi Emmanuel Yahana amesema mradi huo
umetekeleza kigezo namba 2.2 cha Mwenge wa Uhuru na sera ya barabara na mradi
ulianza kutekelezwa Agosti 16 mwaka 2024 ukitarajiwa kukamilika Octoba 2025.
Amesema mradi huo unazisaidia kata hizo kufuata huduma
katika Halmashauri ya Bukoba huku
akitaja uwepo wa ongezeko la majengo ya kibiashara katika eneo hilo na
kupunguza changamoto ya wananchi kuzunguka kuzifikia kata hizo huku wengine
wakitumia gharama nyingi Kufika katika Ofisi za Mkurugenzi Mtendaji wa
halmashauri ya Bukoba.
"Mradi huo umetekelezwa kwa awamu 4 na sasa tunaendelea vizuri ambapo
sasa katika hatua zote za utekelezaji ni kumrahisishia mwananchi kupata huduma
na katika maeneo haya tumeanza kushuhudia ujenzi wa maduka na ongezeko la
wakazi wakati zamani hata barabara ilikuwa haipitiki," alisema Yohana.
Baadhi ya Wananchi wa Kata ya Katerero Halmashari ya Bukoba
Mkoani Kagera wameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwajengea mradi
barabara hiyo kwani kwa sasa hawana hofu na vyombo vyao vya Usafiri.
Mbio za Mwenge wa
Uhuru mwaka 2025 imeweka jiwe la Msingi
katika mradi huo ambao unaendelea kutekelezwa kwa viwango huku watumishi
wa jengo jipya La Halmashauri mpya Ya
wilaya ya Bukoba wakishuhudia lami hadi mlangoni kwao.
Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa ndugu Ismail Ussi ameipongeza TARURA kwa usimamizi na utekekezaji barabara na kuwataka wananchi waendelee kutunza miundombinu ya barabara na kufanya uwekezaji kwani uwepo wa barabara unarahisisha Mawasiliano.
0 Maoni