Mhandisi Mativila akagua mradi wa lami ya RTC-Sungura

 

Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu Mhandisi Rogatus Mativila yupo Wilayani Ukerewe kwa ziara ya kikazi.

Katika ziara hiyo Mhandisi Mativila alipokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Wilaya hiyo  Mhe. Christopher Ngubiagai.

Mhandisi Mativila ametembelea na kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami ya RTC-Sungura yenye urefu wa Km 0.321 pamoja na barabara ya Pump House Km 0.299 katika mji wa Nansio.




Chapisha Maoni

0 Maoni