Maporomoko yaua watu wapatao 1,000 Sudan

 

Maporomoko ya ardhi yameua watu wapatao 1,000 katika eneo la mbali la Milima ya Marra, magharibi mwa Sudan, kwa mujibu wa kundi la waasi la Jeshi la Ukombozi wa Sudan (Sudan Liberation Movement Army).

Mvua kubwa zilizonyesha kwa siku kadhaa zilisababisha maporomoko hayo siku ya Jumapili, na kundi hilo limesema katika taarifa kuwa mtu mmoja tu ndiye aliyenusurika na kuwa kijiji cha Tarasin "kimesawazishwa kabisa".

Kundi hilo limeomba msaada wa kibinadamu kutoka kwa Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kikanda na kimataifa.

Wakazi wengi wa jimbo la Darfur Kaskazini walikimbilia eneo la Milima ya Marra kutafuta hifadhi, baada ya vita kati ya jeshi la Sudan na kikosi cha wanamgambo cha Rapid Support Forces (RSF) kupelekea kuzikimbia nyumba zao.

Chapisha Maoni

0 Maoni