Katibu
Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, amesema Hifadhi ya
Wanyamapori Makuyuni inayojulikana kama Makuyuni Wildlife Park ni hifadhi mpya
ya kimkakati, inayofikika kwa urahisi na inayompa fursa mtalii wa kuona
wanyamapori kwa ukaribu zaidi na kwa muda mfupi.
Dkt.
Abbasi ameyasema hayo leo Septemba 28,2025, alipotembelea Hifadhi ya
Wanyamapori Makuyuni ikiwa ni muendelezo wa ziara ya kikazi katika maeneo
yanayosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).
Aidha,
Dkt. Abbasi ameongeza kuwa kutokana na upekee wa Hifadhi hii, amesisitiza
kuendelea kubuniwa kwa mazao mengi ya utalii ili kumpa mtalii fursa ya kufanya
shughuli mbalimbali za utalii akiwa ndani ya hifadhi.
Kwa
upande wake, Kaimu Kamishna wa Uhifadhi - TAWA, Mlage Yussuf Kabange amesema
kuwa, TAWA imeboresha miundombinu iliyopo katika Hifadhi ya Wanyamapori
Makuyuni, ikiwemo ujenzi wa bwawa la kukusanyia maji kwa ajili ya wanyamapori,
ujenzi wa barabara na vivuko vinavyoifanya hifadhi iweze kufikika katika majira
yote ya mwaka.
Sambamba
na hilo, Kamishna Kabange amesema kuwa TAWA inaendelea na jitihada za kutangaza
utalii na kuvutia wawekezaji ili wawekeze katika maeneo mbalimbali
yanayosimamiwa na TAWA.
Awali,
akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi wa Makuyuni Wildlife Park, Afisa Mhifadhi
Ruahamangi Kishe, amesema Hifadhi ya Makuyuni imesheheni vivutio mbalimbali
wakiwemo wanyamapori kama vile Tembo, Simba, Twiga, Choroa, Pundamilia, Nyati
na Pofu. Pia hifadhi ya Makuyuni imezungukwa na jamii ya kimasai inayotoa fursa
ya kufanya utalii wa kiutamaduni.
Makuyuni
Wildlife Park inapatikana Wilaya ya Monduli, takribani kilometa 40
kutoka Arusha Mjini.
Na. Joyce
Ndunguru, Arusha.




0 Maoni