Kapteni Abbas Ali Mwinyi kuzikwa kesho Mangapwani

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt Hussein Ali Hassan Mwinyi ametangaza kwa masikitiko kutokea kifo cha Kaka yake Kapteni Abbas Ali Hassan Mwinyi aliyefariki dunia leo 25 Septemba 2025 Mjini Unguja, Zanzibar.

Ibada ya kumsalia Marehemu itafanyika katika Msikiti wa Zanzibar - Msikiti wa Qaboos baada ya sala ya Ijumaa na baada ya hapo maziko yanafanyika Mangapwani katika eneo ambalo amezikwa Mzee Ali Hassan Mwinyi, ambapo watu waliopo maeneo ya Mangapwani, Bumbwini, Fujoni na maeneo ya karibu watapata kutabaruku kabla ya kuzika.

Visomo Msikitini vitaanza saa 4 asubuhi.

Kapteni Abbas Ali Mwinyi alikuwa mbunge aliyemaliza muda wake na mgombea wa jimbo la Fuoni kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Chapisha Maoni

0 Maoni