Kampeni za Shigongo Buchosa nyumba kwa nyumba

 

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Buchosa, Eric Shigongo, amefanya kampeni za nyumba kwa nyumba ili kutafuta kura za kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na wabunge na madiwani, ili waweze kuwaletea wananchi maendeleo.

Kampeni hizo zimefanyika katika Kijiji cha Kakobe, Kata ya Kazunzu, kabla ya uzinduzi rasmi wa kampeni uliofanyika katika Kijiji cha Nyambeba, Jimbo la Buchosa.

Shigongo amewaomba wananchi wa Buchosa kushirikiana kwa pamoja katika kutafuta kura za rais, wabunge na madiwani wanaotokana na CCM, kwa lengo la kuhakikisha chama hicho kinashinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu.

Amesema wagombea wa CCM ndiyo chaguo bora kwa Watanzania kutokana na kazi nzuri zilizofanywa na serikali ya CCM na zinazondelea kufanyika, hivyo kuna sababu ya kuendelea kukiunga mkono chama hicho ili kiendelee kuiongoza Tanzania.



Chapisha Maoni

0 Maoni