Dkt. Nchimbi atinga jimbo la Lupembe, Njombe

 

Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi amewahutubia wananchi  wa jimbo la Lupembe, waliohudhuria mkutano wake mdogo wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa mpira wa Ilunda, Lupembe leo Jumatano Septemba 24, 2025 mkoani Njombe.

Pamoja na mambo mengine Dkt. Nchimbi alitumia mkutano huo kuwanadi mgombea ubunge wa jimbo la Lupembe kwa tiketi ya CCM, Ndugu Edwin Enosy Swallel Swallel pamoja na madiwani wa jimbo hilo.

Dkt. Nchimbi anaendelea na mikutano yake ya kampeni nchi nzima, kusaka kura za ushindi wa kishindo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwaombea kura Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wabunge na Madiwani.


Chapisha Maoni

0 Maoni