Wenyeviti Bodi ya TANAPA, NGORONGORO, TAWA, na TFS wakutana

 

Wenyeviti wa Bodi za Taasisi za Uhifadhi zinazounda Jeshi la Uhifadhi  wa Wanyamapori na Misitu Tanzania wakiongozwa na Mwenyekiti wao Jenerali (Mstaafu) George M. Waitara (Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini TANAPA) wamekutana leo Agosti 4, 2025 Jijini, Dar es Salaam katika kikao cha kawaida cha kujadili mwenendo wa Jeshi la Uhifadhi na Misitu Nchini.

Kikao hicho pia, kimehudhuriwa na Jenerali (Mstaafu) Venance S. Mabeyo (Mwenyekiti wa Bodi ya Ngorongoro), Meja Jenerali (Mstaafu) Hamis R.Semfuko (Mwenyekiti wa Bodi ya TAWA) pamoja na Meja Jenerali Mbaraka N. Mkeremi (Mwenyekiti wa Bodi ya TFS).

Aidha, pamoja na Wenyeviti hao, kikao hicho kilihudhuriwa pia na Kamishna wa Uhifadhi - TFS Prof. Dosantos Silayo, Kamishna wa Uhifadhi - TANAPA, Musa Nassoro Kuji, Kamishna wa Uhifadhi - Ngorongoro, Abdul- Razaq Badru, Kaimu Kamishna wa Uhifadhi - TAWA, Mlange Kabange pamoja na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Fidelis Ignas Kapatala ambaye ni Mratibu wa Jeshi la Uhifadhi na Misitu katika Wizara ya Maliasili na Utalii.


Chapisha Maoni

0 Maoni