Bukombe wamchagua Dkt. Doto Biteko kwa 99.8%

 

Wajumbe wa Mkutano Mkuu na Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Bukombe wamemchagua mtia nia wa jimbo hilo Dkt. Doto Mashaka Biteko kwa asilimia 99.8 baada ya kupata kura 7,441 kati ya kura 7,456 zilizopigwa ili apeperushe bendera ya Chama hicho.

Akitangaza matokeo hayo Agosti 04, 2025 Msimamizi wa uchaguzi amesema kuwa Jimbo la Bukombe linajumla ya wajumbe 7,835 na waliopiga kura ni 7,456 ambapo kura zilizoharibika ni 15, kura za hapana ni 0, kura halali zilizopigwa ni 7,441.

Kwa matokeo hayo, Dkt. Doto Mashaka Biteko amepata kura 7,441 kati ya 7,456 sawa na wastani wa asilimia 99.8 uchaguzi uliofanyika katika Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita.

Chapisha Maoni

0 Maoni