Wananchi wajionea live vivutio vya utalii banda la NCAA Nane Nane

 

Wananchi wameendelea kumiminika katika banda la Mamlaka ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) katika maonesho ya Nane Nane Jijini Dodoma kupata elimu ya vivutio vya utalii, taratibu za kuingia hifadhini pamoja na huduma mbalimbali zinazopatikana katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.

Katika maonesho hayo wageni mbalimbali wanaotembelea banda la Wizara ya Maliasili na Utalii katika maonesho ya Nanenane Dodoma wamepata fursa ya kushuhudia vivutio vya utalii moja kwa moja kutokea Hifadhi ya Ngorongoro kupitia "TV Screen" kubwa iliyofungwa katika banda la Wizara hiyo.

Maonesho ya Nane Nane yalianza Agosti 1,2025 na yanatarajiwa kufika kilele chake Agosti 8,2025 yenye kauli mbiu " Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025".

 

Chapisha Maoni

0 Maoni