Vyombo vya habari vyaaswa kutumia Akili Unde kwa uadilifu

 

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Viongozi Wanawake (WPL), Bi. Neema Lugangira amevitaka vyombo vya habari nchini  vitumie Akili Unde kwa uadilifu na isiwe silaha ya kupotosha demokrasia katika kipindi cha uchaguzi mkuu nchini.

Bi. Lugangira ambaye anaitumikia Jumuiya hiyo inayohusisha Marais, Makamu wa Rais, Mawaziri Wakuu, Mawaziri, Wabunge na Mameya, yenye maskani yake Brussels nchini Ubelgiji, ametoa kauli hiyo leo kwenye Mkutano wa Wanachama wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Amesema kwamba Akili Unde imeleta changamoto za Deepfakes (picha na video bandia) zinazoweza kuharibu heshima ya mgombea,  Bots (roboti) zinazopandikiza maoni bandia pamoja na mashambulizi ya matusi na ukatili wa kijinsia mtandaoni.

Hata hivyo, amesema  Akili Unde pia ni fusa inaweza kutumika vizuri kama kutumika kufuatilia mwenendo wa hate speech (kauli za chuki) mtandaoni, kusaidia kuzuia upotoshaji wa uchaguzi.

“Akili Unde pia Inaboresha ushirikishwaji wa wapiga kura na elimu, kwa kutoa taarifa kwa urahisi kuhusu mchakato wa uchaguzi, sheria, na wagombea kwa kutumia roboti za mazungumzo (chatbots),” alisema Lugangira.

Ameongeza kuwa Akili Unde inasaidia kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wapiga kura wa makundi maalum, kama vile walemavu na vijana, kwa kutumia teknolojia ya sauti na huduma za kielektroniki.

Pamoja na mambo mengine, amesema Akili Unde pia inaweza kuboresha mikakati ya kampeni kwa kutumia uchambuzi wa data ya wapiga kura na kufanya matangazo ya kisiasa kuwa ya kulenga na yenye ufanisi.

Bi. Lugangira amesema vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kulinda uchaguzi dhidi ya matumizi mabaya ya teknolojia kwa pamoja na kuhakikisha kuwa wanawake wanapewa fursa sawa, ukosefu wa usawa na ukatili wa kijinsia unaoripotiwa na kushughulikiwa.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Viongozi Wanawake (WPL), Bi. Neema Lugangira akiwakabidhi  nakala za Mwongozo wa Uchaguzi Afrika wa Mitandao ya Jamii kwa Mwenyekiti wa TEF Deodatus Balile na Makamu Mwenyekiti Dkt. Bakari Machumu.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Viongozi Wanawake (WPL), Bi. Neema Lugangira akiwakabidhi  nakala za Mwongozo wa Uchaguzi Afrika wa Digitali na Mitandao ya Jamii kwa Mwenyekiti wa TEF Deodatus Balile na Makamu Mwenyekiti Dkt. Bakari Machumu.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Viongozi Wanawake (WPL), Bi. Neema Lugangira akiwakabidhi  nakala za Mwongozo wa Uchaguzi Afrika wa Digitali na Mitandao ya Jamii kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) Dkt. Rose Rueben na aliyekuwa Mwenyekiti wa TAMWA Bi. Joyce Shebe.

Chapisha Maoni

0 Maoni