TFS yapelekea Wizara ya Maliasili na Utalii kupata tuzo

Makamu wa Rais Mhe. Philip Isdor Mpango amekabidhi tuzo kwa Wizara  ya Maliasili na Utalii kufuatia utendaji mzuri wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), tuzo ambayo imepokelewa na Naibu Waziri Mhe. Dunstan Kitandula kwa niaba ya Mhe. Pindi Hazara Chana, Waziri wa Maliasili na Utalii.

Tuzo hiyo imetolewa kwenye ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Majadiliano wa Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Serikali ulioandaliwa na Msajili wa Hazina katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano Arusha.





Chapisha Maoni

0 Maoni