Mke wa Rais anayetumikia kifungo akamatwa Korea Kusini

 

Mke wa rais wa zamani wa Korea Kusini aliyefungwa, Yoon Suk Yeol, amekamatwa kwa mashtaka kadhaa, ikiwa ni pamoja na udanganyifu wa hisa pamoja na rushwa.

Aliyekuwa mama wa taifa, Kim Keon Hee, alikana mashtaka yote wakati wa kikao cha saa nne cha Mahakama kilichofanyika mjini Seoul siku ya Jumanne.

Hata hivyo, Mahakama ilitoa hati ya kumuweka kizuizini, ikitaja uwezekano wa yeye kuharibu ushahidi.

Korea Kusini ina historia ya marais wa zamani kufunguliwa mashtaka na kufungwa jela. Hata hivyo, hii ni mara ya kwanza kwa rais wa zamani pamoja na mkewe wote wawili kufungwa.

Yoon alikamatwa mwezi Januari ili kufikishwa mahakamani kwa jaribio la kutekeleza sheria ya kijeshi lililoshindikana mwaka jana, ambalo liliingiza nchi katika machafuko na hatimaye kusababisha kuondolewa kwake madarakani.

Rais wa zamani wa Korea Kusini aliyefungwa, Yoon Suk Yeol akiwa na mkewe Kim Keon Hee wakati akiwa madarakani kama Rais wa Korea Kusini.

Chapisha Maoni

0 Maoni