Kumbilamoto achukua fomu za kugombea udiwani Vingunguti

 

Mgombea Udiwani  wa Kata ya Vingunguti Kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Omary Kumbilamoto  ambae anatetea nafasi hiyo leo amechukua fomu ya kugombea  kiti hicho katika ofisi ya Kata ya Vingunguti.

Kumbilamoto ambaye alisindikizwa na umati mkubwa wa watu aliweza kuchukua fomu hiyo Majira ya saa 9:40 asubuhi chini ya uangalizi wa katibu Kata Wa CCM Mama Agatha.

Mara baada ya kuchukua fomu hiyo Kumbilamoto alijinasibu Kwa kusema kuwa anaimani kubwa ya kushinda uchaguzi huo kutokana utekelezaji mkubwa wa ilani uliofanyika katikati kata ya  Vingunguti.

"Katika miaka mitano tuliyopewa dhamana na wana Vingunguti CCM tumefanya makubwa mengi kuanzia miundombinu ya barabara, masoko,huduma za Afya na kuwafikia wananchi mmoja mmoja katika mahitaji yao," amesema Kumbilamoto.

Ametaja Kuwa katika miaka yake mitano ya Udiwani amewezesha kupatikana kwa Ambulance katika zahanati ya Vingunguti, Soko la kisasa la nyama Choma, Machinjio na Mabucha ya Kisasa pamoja na barabara za zege mitaani.

Amesema kuwa CCM inakaribisha wagombea wa vyama vya upinzani kuweka wagombea wao waje washindane kwa hoja sio matusi.



Chapisha Maoni

0 Maoni