Hospitali ya Taifa
Muhimbili Upanga na Mloganzila kwa kushirikiana na Vodacom Tanzania Foundation
imehitimisha kambi ya ya siku sita katika mikoa ya Tanga na Kilimanjaro kuanzia
tarehe 21 hadi 27 Julai, 2025 ambapo katika kambi hiyo wananchi takribani 3,800
wamenufaika na huduma za uchunguzi na matibabu ya kibingwa na ubingwa bobezi
bure.
Katika kambi hiyo
wananchi waliofanyiwa uchunguzi na matibabu ya macho ni 1,499 Magonjwa ya ndani
1,207, Afya ya kina mama na uzazi 867, Masikio, Pua na Koo 803, tathmini ya
watu wenye ulemavu 813, huduma ya afya ya watoto 700, Afya ya Kinywa na Meno
671, Saratani 756, Ngozi 621 na afya ya akili 553.
Aidha kati ya wagonjwa
1,499 waliofanyiwa uchunguzi wa macho walibainika kuwa na changamoto mbalimbali
ikiwemo ukavu wa macho, mzio, uoni hafifu, kushindwa kusoma maandishi madogo ya
karibu, mtoto wa jicho na shinikizo la macho.
Akielezea sababu kubwa
inayochangia watu kupata changamoto za macho katika maeneo hayo, Daktari Bingwa
wa Macho, Dkt. Joachim Kilemile amesema ni uzee, kisukari pamoja na shinikizo
la juu la damu.
Hospitali ya Taifa
Muhimbili Upanga na Mloganzila katika jitihada zake za kuendelea kusogeza
huduma karibu na wananchi inatarajia kufanya huduma mkoba (outreach) katika
Viwanja vya Nane Nane mkoani Dodoma kuanzia Agost 1 hadi 8, 2025.
0 Maoni