Songea, nyumbani kwa Mashujaa wa Majimaji

 

Mji wa Songea unasimama kama ngome ya kihistoria, ukihifadhi kumbukumbu ya mashujaa waliomwaga damu yao kupigania uhuru wa Tanganyika kupitia Vita ya Majimaji (1905–1907) — vita ya kwanza kubwa ya kisasa ya waafrika dhidi ya ukoloni barani Afrika!

Mashujaa 67 walinyongwa kwa kosa moja: KUPINGA UKOLONI!

Mashujaa 66 walizikwa kwenye kaburi moja—ishara ya mshikamano wa kweli. Na shujaa mkuu, Nduna Songea Mbano, alizikwa peke yake kwa heshima kubwa. Leo, kaburi lake linaheshimiwa ndani ya Makumbusho ya Majimaji, makumbusho pekee nchini Tanzania yanayohifadhi urithi halisi wa vita vya ukombozi.

Jina la Songea linabeba urithi wa Nduna Songea Mbano, shujaa wa kweli. Kupitia historia hii ya kipekee, Songea inajitokeza kama kituo muhimu cha utalii wa kihistoria na kiutamaduni.

Chapisha Maoni

0 Maoni