CCM yavuna sh bilioni 2.7 ada fomu za ubunge

 

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeingiza kiasi cha shilingi 2,737,500,000 kutokana na ada za fomu za kuwania ubunge.

Kiasi hicho cha fedha kimetokana na ada za watia nia 5,475 waliochukua fomu za kuwania ubunge katika majimbo mbalimbali. Ada ya fomu moja ni shilingi 500,000.

Kiasi hiki kinadhihirisha mshikamano na hamasa kubwa ya wanachama wa CCM kushiriki mchakato wa uchaguzi wa ndani wa chama, ambao ni hatua muhimu kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

CCM imeendelea kusisitiza umuhimu wa mchakato wa uchaguzi ndani ya chama kufanyika kwa uwazi na haki ili kuhakikisha wagombea bora na wenye sifa wanapata nafasi ya kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

Chapisha Maoni

0 Maoni