Waziri Mkuu mgeni rasmi Maadhimisho ya Miaka 20 ya MUM

 

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Juni 20, 2025  amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM), kwenye viwanja vya chuo hicho mkoani Morogoro.

Maadhimisho hayo ni jukwaa la kutathmini historia, changamoto, mafanikio yaliyopatikana na mchango wa chuo hicho katika maendeleo ya Taifa.

Pia, Maadhimisho hayo yamelenga kuakisi changamoto na maendeleo ya chuo hicho katika kipindi cha  miaka 20 ya kutoa maarifa, nidhamu, na malezi bora ya vijana wa Kitanzania



Chapisha Maoni

0 Maoni