Waziri Dkt. Pindi Chana mgeni rasmi Tuzo za Utalii za Dunia kanda ya Afrika

 

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe; Balozi. Dkt Pindi H. Chana (Mb) anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika tukio la kihistoria la utoaji wa tuzo za Utalii duniani kanda ya afrika ambazo zitafanyika leo tarehe 28 Juni, 2025 katika Hoteli ya hadhi ya nyota tano ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam.

Hafla hiyo inayotarajiwa kuanza saa 12:30 za jioni na kuisha 05:00 za usiku itahidhuriwa pia na viongozi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe; Dunstan Kitandula (Mb), Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt Hassan Abbas, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe; Albert chalamilla, viongozi wa vyombo  vya Ulinzi nchini pamoja na viongozi wa taasisi mbalimbali za Serikali na sekta binafsi.

Katika tukio hilo,  zaidi ya washiriki 500 kutoka mataifa mbalimbali watahudhuria ambapo tukio hilo pia  litakuwa mubashara (Live) kupitia vyombo vya habari mbalimbali  ili kuwezesha watanzania na watu wengine  ulimwenguni  kufuatilia tukio hilo adhimu na la kihistoria hapa nchini.

Vyombo vya habari ambavyo vitarusha tukio hilo mubashara ni pamoja na Tanzania Safari Channel, Azam TV, ITV, ZBC, Tbc Digital, Utalii TV, Clouds TV, Tanzania Unforgettable, Tanzania Parks na mitandao ya kijamii mbalimbali.

Chapisha Maoni

0 Maoni