Bei ya mafuta duniani zinatarajiwa kupanda pale masoko ya nishati yatakapoanza kufanya biashara siku ya Jumatatu asubuhi huko Asia, kufuatia shambulio la Marekani dhidi ya Iran.
Taarifa kutoka katika
masoko ya kimataifa zinaonyesha kuwa bei ya mafuta aina ya Brent ilifunga wiki
ya biashara siku ya Ijumaa kwa dola 77.01 kwa pipa, ikiwa ni ongezeko la karibu
asilimia 20 ndani ya kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
Hata hivyo, wataalamu
wa masoko wanasema kuwa pamoja na ongezeko hilo la bei, bado kiwango hicho kiko
chini ya bei zilizoshuhudiwa katika kipindi kama hiki mwaka uliopita.
Gharama ya mafuta
ghafi huathiri mambo mengi, kuanzia kiasi cha pesa unachohitaji kujaza gari lako
mafuta hadi bei ya vyakula kwenye maduka makubwa ya rejareja.
Ongezeko la bei ya
mafuta ghafi lina madhara makubwa kwa uchumi wa kila siku, hasa kwa nchi
zinazoagiza mafuta kutoka nje, kama Tanzania.
Mabadiliko ya bei ya
mafuta huathiri moja kwa moja gharama za usafirishaji, uzalishaji viwandani, na
bei za bidhaa muhimu kama vyakula, mbolea na huduma nyinginezo.
Kwa takwimu za 2023 Iran
ilikuwa nchi ya 7 kwa ukuzaji wa mafuta ghafi duniani ikiwa na uzalishaji wa takriban
mapipa 3.94 milioni ya mafuta kwa siku.
0 Maoni