Twiga Minerals Corporation kinara wa kuchangia gawio 2025

 

Kampuni ya Twiga Minerals Corporation imekuwa kinara katika kuchangia gawio kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali kwa kampuni za biashara ambapo imetoa gawio la shilingi bilioni 93.6.

Kampuni ya Airtel Tanzania imekuwa mchangiaji wa pili kwa kuchangia fedha kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali ambapo imetoa gawio la shilingi bilioni 73.9

Nafasi ya tatu imechukuliwa na Benki ya NMB kwa kutoa gawio la shilingi bilioni 68.1

Kampuni zingine zilizotoa gawio kubwa mwaka huu chini ya taasisi zilizotajwa hapo juu ni pamoja na Kampuni ya Puma Energy iliyotoa gawio la shilingi bilioni 13.5.

Nyingine ni Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) iliyotoa gawio la shilingi bilioni 11 pamoja Benki ya Kitaifa ya Biashara NBC iliyotoa gawio la shilingi bilioni 10.5.

Hayo yamebainika leo Juni 10, 2025, Ikulu, Dar es Salaam, wakati wa hafla ya kupokea gawio na michango kutoka kwa mashirika na taasisi za umma ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Chapisha Maoni

0 Maoni