Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Kanali Mstaafu Evans Mtambi, leo amezindua rasmi shule mpya ya sekondari ya Muhoji iliyopo katika Kijiji cha Muhoji, Kata ya Bugwema, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.
Uzinduzi huo
umefanyika mbele ya mamia ya wananchi wa Kata ya Bugwema inayojumuisha vijiji
vinne vya Bugwema, Kinyang’erere, Masinono na Muhoji, ambapo shule hiyo mpya
inakuwa sekondari ya pili katika kata hiyo.
Akizungumza katika
hafla hiyo, Mhe. Mtambi amesema ujenzi wa shule hiyo ni ushahidi wa dhamira ya
dhati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya
kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya elimu nchini.
“Tunamshukuru
Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuboresha mazingira ya utoaji elimu kwa
Watanzania wote. Hii ni sehemu ya juhudi za Serikali kupeleka maendeleo hadi
ngazi ya kijiji,” alisema RC Mtambi.
Wananchi wa Kata ya
Bugwema pamoja na viongozi wao walitumia jukwaa hilo kueleza kwa sauti moja
kuwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ndiye chaguo lao pekee kuendelea kuiongoza
nchi kutokana na kazi kubwa anayofanya hususan kwenye sekta ya elimu.
Ujenzi wa shule hiyo
ulianza mwezi Desemba 2022 kupitia michango mbalimbali iliyokusanywa kwenye
harambee iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Profesa Sospeter
Muhongo.
Kwa mujibu wa taarifa
ya Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo ujenzi, shule
hiyo umegharimu jumla ya Shilingi 175,346,955 hadi hatua iliyofikiwa, huku
0 Maoni