Serikali imefunga
shughuli za Kanisa la Glory of Christ Church maarufa kama Kanisa la Ufufuo na
Uzima linaloongozwa na Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima kwa kutoa
mahubiri yenye mwelekeo wa kisiasa na nia ya kuichonganisha serikali na
wananchi.
Taarifa aliyoitoa leo
Msajili wa Jumuiya za Kiraia Emmanuel Kihampa na nakala kwenda kwa Mkuu wa
Jeshi la Polisi (IGP) Camillus Wambura, imesema vitendo hivyo ni kinyume cha
Sheria ya Jumuiya Sura ya 337 na vinaweza kuhatarisha amani na utulivu nchini.
0 Maoni