Rais Samia azungumza na DG mpya wa TRC

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu Mteule wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Mhandisi Machibya Shiwa, mapema leo Juni 26, 2025 kabla Mheshimiwa Rais hajasafiri na Treni ya SGR kwenda Dodoma.

Hii ni mara ya kwanza kwa Mkurugenzi Mkuu mteule wa TRC Mhandisi Machibya, kukutana na Mhe. Rais Samia akiwa katika wadhifa wake mpya toka ateuliwa na Mheshimiwa Rais kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TRC Juni 23, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekea Jijini Dodoma ambapo Pamoja na mambo mengine kesho Juni 27, 2025 anarajiwa kuhutubia na kuhitimisha shughuli za Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Chapisha Maoni

0 Maoni