Waziri wa Maliasili
na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) Juni 25, 2025 alitembelea Ofisi ya
Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo iliyopo Zanzibar na
alipokelewa na mwenyeji wake, Katibu Mkuu wa wa Wizara hiyo Ali Khamis Juma.
Waziri Chana
aliambatana na Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori
Tanzania (TAWA) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mej. Jen (Mstaafu) Hamis
Semfuko.
Mazungumzo kati ya
Waziri Chana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na
Mifugo, Ali Khamis Juma yalijikita katika maeneo mbalimbali yakiwemo kupanga
mikakati ya kukuza utalii nchini kati ya Wizara hizo mbili pamoja na kuangalia
fursa za uwekezaji wa Bustani ya Wanyamapori Zanzibar iliyopo katika Hifadhi ya
Jambiani Muyuni iliyopo Mkoa wa Kusini.




0 Maoni