Ngorongoro yashinda Tuzo ya Kivutio Bora cha Utalii barani Afrika mwaka 2025

 

Eneo la Hiafadhi ya Ngorongoro limetangazwa na kushinda tuzo ya kuwa kivutio bora cha utalii Barani Afrika kwa mwaka 2025.

Ngororngoro imeibuka kidedea katika tuzo za World Travel Awards (WTA) zilizofanyika jana usiku  tarehe 28 Juni, 2025 katika hoteli ya Johari Rotana Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Pindi Chana.

Ngorongoro imevishinda vivutio vingine vya utalii ambavyo ni  Harbeespoort Aerial Cableway, V & AWaterfront, Table Mountain na Kisiwa cha Robben za Afrika Kusini, Pyramids of Giza ya Misri, ziwa Malawi na Mlima Kilimanjaro.

#TanzaniaShines

#Ngorongoroshines

Chapisha Maoni

0 Maoni