Ajali ya mabasi yahofiwa kusababisha vifo Same

 

Watu kadhaa wanahofiwa kupoteza maisha baada ya kutokea ajali iliyohusisha basi la kampuni ya Channel One lililokuwa likisafiri kutokea Moshi kuelekea Tanga kugongana uso kwa uso na basi dogo aina ya Coaster lililokuwa likitoka wilayani Same.

Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni amesema ajali hiyo imetokea katika eneo la Sabasaba Kata ya Same, wilayani Same, mkoani Kilimanjaro, na magari yote mawili yalilipuka moto na kuteketea.



Chapisha Maoni

0 Maoni