Timu ya Madaktari,
Wauguzi na Wataalamu Mitambo wa Hospitali ya Benjamin Mkapa wako Tokyo nchini
Japan kwa mafunzo maalum ya kuzibua mishipa ya kwenye ubongo na kutanua mishipa
ya kwenye ubongo bila kufungua fuvu la kichwa.
Mafunzo hayo
yanafanyika katika maabara maalumu ya angiosuit Kamagaya General Hospital na
Dokkyo University Hospital za Tokyo nchini Japan.
Kiongozi wa Timu
kutoka BMH ambaye ni Mkurugenzi wa Upasuaji wa BMH Dkt. Henry Humba
amesema kuwa wamepata nafasi ya kujifunza kuzibua mishipa ya damu ya kwenye
ubongo “ thrombectomy” na pia kutanua mishipa ya damu ya kwenye ubongo kwa
kuweka stenti “ carrotid stenting”, pia kuzuia sehemu za mishipa ya damu
zilizovimba/ kupasuka (aneurysms) na kuziba mishipa ya damu inayoenda kwenye
Vimbe za kwenye ubongo ( brain tumor embolization).
"Hii ni
maandalizi kwa ajili ya kutoa huduma hii hapo BMH na pia huduma hii ni
kipaumbele cha wizara ya afya kwa mwaka ujao wa fedha na fursa hii ya mafunzo
yanayotarajiwa kukamilika baadae mwezi Juni, imepatikana kutokana na
mashirikiano kati ya BMH na Tokushukai Medical Group ya nchini Japan,”
alimalizia Dkt. Humba.
Nae Mkuu wa Idara ya
Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya fahamu Hospital ya chuo Kikuu cha Dokkyo
iliyopo Tokyo nchini Japan Prof. Kensuke Suzuki amesema kuwa tangu
mwezi Mei mwishoni wamekuwa na timu ya wataalamu wa mishipa ya fahamu kutoka
BMH Tanzania imekuwa ikitembelea idara yao na kufanya mafunzo, kwa kipindi
chote hicho wamepata fursa ya kubadilishana utaalamu na uzoefu.
0 Maoni