Bilionea Elon Musk
amesema anajutia baadhi ya kauli alizozitoa dhidi ya Rais wa Marekani, Donald
Trump, kufuatia mvutano wao wa maneno uliotokea kwenye mitandao ya kijamii wiki
iliyopita.
Kupitia mtandao wake
wa kijamii, X (zamani Twitter), Musk aliandika:
"Ninajutia
baadhi ya machapisho yangu kuhusu Rais Donald Trump wiki iliyopita. Nilikwenda
mbali kupita kiasi."
Kauli hiyo imekuja
siku chache baada ya mvutano wao kufikia kilele, ambapo mmiliki huyo wa kampuni
ya Tesla aliuita muswada wa rais Trump kuwa “aibu na wa kuchukiza” maneno
yaliyosababisha mvutano mkubwa wa kisiasa.
Rais Trump, kwa
upande wake, alijibu vikali kwa kusema kuwa uhusiano wake na Musk umefikia
kikomo na hana mpango wowote wa kuurekebisha.
Kabla ya mvutano huo,
Musk alikuwa miongoni mwa wafadhili wakubwa wa kampeni ya Trump ya kugombea
urais mwaka 2024, na alikuwa akionekana kama mshirika wake wa karibu kisiasa.
Katika hatua nyingine
kali, aliyekuwa mshauri wa Trump, Steve Bannon, alimtaka Musk, ambaye ni
mzaliwa wa Afrika Kusini, arejeshwe nchini kwake akidai amekuwa "tisho kwa
usalama wa taifa".
0 Maoni