Daktari ambaye watoto wake tisa waliuawa katika shambulizi la Israel, afariki

 

Daktari wa Kipalestina ambaye watoto wake tisa waliuawa katika shambulio la anga la Israel huko Gaza tarehe 23 Mei, amefariki dunia kutokana na majeraha aliyopata katika shambulio hilo hilo, maafisa wa afya wamesema.

Dkt. Hamdi al-Najjar alikuwa amerudi baada ya kumpeleka mkewe, Dkt. Alaa al-Najjar, katika Hospitali ya Nasser, ambako wote wawili walikuwa wakifanya kazi, wakati nyumba yao huko Khan Younis ilipopigwa bomu. Watoto wao tisa waliuawa, huku mtoto wa kumi akijeruhiwa vibaya.

Hamdi alilazwa hospitalini na kutibiwa kutokana na majeraha ya ubongo na ya ndani, lakini alifariki dunia siku ya Jumamosi. Alaa na mtoto wao wa kiume mwenye umri wa miaka 11, Adam, ambaye bado yuko hospitalini, ndio waliobaki hai katika familia hiyo.

Chapisha Maoni

0 Maoni