CCM yawalilia watu 28 waliokufa kwenye ajali Mlima Iwambi

 

Chama cha Mapinduzi (CCM), kimetuma salamu za pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera na familia zilizopoteza watu 28 na wengine saba kujeruhiwa katika ajali iliyotokea Mlima Iwambi jijini Mbeya.

Salamu hizo za pole zimetolewa katika taarifa iliyotolewa leo Jumapili Juni 8,2025 na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makalla, ambayo imesema CCM inaungana na Watanzania wote kuwaombea marehemu wapumzike kwa amani.



Chapisha Maoni

0 Maoni