Nguli wa fasihi Ngũgĩ wa Thiong'o afraiki dunia

 

Nguli wa fasihi ya Kingereza Ngũgĩ wa Thiong'o, raia wa Kenya amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 87.

Ngũgĩ alitazamiwa kushinda Tuzo ya Nobel ya Fasihi mara nyingi, na kuwaacha mashabiki wakiwa na masikitiko kila mara tuzo hiyo alipoikosa.

Atakumbukwa si tu kama mwandishi aliyestahili Nobel, bali pia kama mtetezi shupavu wa fasihi iliyoandikwa kwa lugha za asili za Kiafrika.

Ngũgĩ alizaliwa kwa jina James Thiong’o Ngũgĩ mwaka 1938, wakati Kenya ilikuwa chini ya utawala wa kikoloni wa Waingereza.

Alikulia katika mji wa Limuru miongoni mwa familia kubwa ya wafanyakazi wa kilimo wa kipato cha chini.

Chapisha Maoni

0 Maoni