Andikeni habari zitakazosaidia wananchi kuchagua viongozi waadilifu

 

Kamishna wa Maadili Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Mhe. Jaji ( Mst.) Sivangilwa S. Mwangesi amewataka waandishi wa habari kuzingatia weledi wa taalumu yao kwa kutoa taarifa stahiki, zenye ulinganifu zitakazosaidia wananchi kuwachagua viongozi waadilifu.

“Sote tunafahamu kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani baada ya uchaguzi tutapata viongozi watakaoliongoza taifa hili kwa kipindi cha miaka mitano,  hivyo ni muhimu wananchi kuwachagua viongozi waadilifu,” alisema Jaji Mst. Mwangesi.

Jaji Mst. Mwangesi ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam, katika mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari wenye lengo la kuwaelewesha shughuli mbalimbali zinazofanywa na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Ameeleza kuwa juhudi za wahariri katika ukuzaji wa maadili ya viongozi nchini zinaonekana wazi kwa jinsi wanavyotumia kalamu zao kuelimisha, kuhabarisha, kuburudisha na kukosoa jamii kuhusu dhana ya uadilifu kwa viongozi.

Ametoa raia kwa waandishi wa habari kuendelea kutoa habari zinazohusu mienendo ya viongozi wa umma ili wale wenye mienendo isiyofaa waweze kupata kujirekebisha ama wapate kuonywa na mamlaka zinazowasimamia.




Chapisha Maoni

0 Maoni