TBS wameshindwa udhibiti Usalama wa Chakula - Mhe. Lugangira

 

Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Neema Lugangira amependekeza suala la udhibiti wa usalama wa chakula kuondolewa katika Shirika la Viwango nchini (TBS) na kuhamishiwa katika Wizara ya Afya.

Mhe. Lugangira ametoa ushuri huo Bungeni Jijini Dodoma wakati akichangia Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ambapo amesema kwa sasa shirika la TBS limeshindwa kudhibiti suala la usalama wa chakula.

“Kwa sasa Shirika la Viwango TBS limeshindwa kudhibiti usalama wa chakula, tunapaswa kuacha kulifanya suala la chakula kuwa la kibishara…hivyo basi napendekeza suala la udhibiti wa usalama wa chakula lihamishiwe Wizara ya Afya,” amesema Mhe. Lugangira.

Amesema hali ya sasa ya vyakula vinavyotoka ndani na nje vinavyouzwa sokoni hairidhishi,  kwa maana ya usalama wa chakula (food safety). “Hatuwezi kuendelea kufanya suala la usalama wa chakula kibiashara, suala la usalama wa chakula ni suala linalohusu uhai na afya za Watanzania.”

Pamoja na mamo mengine, Mhe. Lugangira ameitaka Serikali kutoa kauli Bungeni ya kuirejesha Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC) kama ilivyoona umhimu wa kurejesha Shirika la Elimu Kibaha, kutokana na umuhimu na uhitaji wa TFNC kwa Watanzania.

Pia, Mhe. Lungangira amependekeza TFNC ihamishiwe kwenye ofisi ya Waziri Mkuu ambaye kwa sasa ofisi yake ndio inaratibu masuala ya lishe kwa sababu suala ya lishe ni suala mtambuka.

Chapisha Maoni

0 Maoni