Rais wa Zambia awaonya mawaziri wala bata

 

Rais wa Zambia Hakainde Hichilema amewaonya mawaziri wanaolala wakati mikutano, jambo ambalo amelihusisha na mienendo yao ya maisha ya kuponda raha bila kujidhibiti.

Hakufafanua zaidi kauli yake hiyo, lakini vyombo vya habari vya nchi hiyo vinaeleza kuwa alikuwa analenga tabia mawaziri za unywaji pombe kupindukia na sherehe za usiku wa manane.

Rais Hichiema ameonya kwamba tabia kama hizo zinaweza kuchangia kuvuja kwa siri za taifa na kupelekea kuchelewesha utoaji huduma za jamii.

Chapisha Maoni

0 Maoni