Rais Samia amnadi Prof. Janabi WHO - Afro

 

Katika kusherehekea Siku ya Afya Duniani leo Aprili 7, 2025, yenye kaulimbiu "Mwanzo Mzuri wa Afya, Mustakabali wenye matumaini", Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amechukua fursa hii kumtangaza na kuunga Mkono Kampeni ya Prof. Mohamed Yakub Janabi kama mgombea kutoka Tanzania kwa nafasi ya Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika (WHO - Afro).

 “Ninaunga mkono maono yake ya kuwa na Afrika yenye afya bora, imara, na yenye mafanikio, ambapo kila mtu atapata huduma bora za afya, na ambapo mifumo ya afya itakuwa imara kukabiliana na changamoto za baadaye,” alisema Mhe. Samia.

“Uzoefu wake na utendaji kazi wake pamoja na mafanikio aliyoyapata yanajieleza yenyewe. Nina imani kwamba, uongozi wake utaleta matokeo chanya ya afya na ustawi wa jumla katika bara letu la Afrika.”

Chapisha Maoni

0 Maoni