TARURA yakutana na Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Dar es Salaam

 

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeendelea kuwajengea uelewa waandishi wa habari wa mkoa wa Dar es Salaam kuhusu mipango na mikakati ya wakala huo.

Akizungumza kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Wakala huo, Meneja wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhandisi Geofrey Mkinga amesema kwamba mkoa wa Dar es salaam katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 imeidhinishiwa jumla ya bilioni 68 kwaajili ya ukarabati na matengenezo ya Barabara Km. 1,151.987 ikiwemo lami Km. 26.04, madaraja na Kalavati 38.

Amesema maendeleo ya utekelezaji kwa Mipango ya mwaka 2024/2025 yanahusisha utekelezaji wa kimaumbile na kifedha ambapo utekelezaji hadi kufikia Disemba 2024 wa kimaumbile ni asilimia 53.

Kwa upande wa mradi wa DMDP-II Mhandisi Mkinga amesema jumla ya zabuni 8 za awamu ya kwanza kati ya hizo, zinajumuisha barabara zenye urefu wa Km. 64 kwa gharama ya bilioni 190 zilisainiwa Oktoba 23, 2024 na miradi hiyo imeanza rasmi tarehe 15 Januari, 2025.

Ameongeza kusema kuwa awamu ya pili Zabuni 9 kati ya hizo, zinajumuisha barabara zenye urefu wa Km. 84.24 kwa gharama ya bilioni 221 zilisainiwa Machi 21, 2025 na Wakandarasi wanaendelea na kazi za awali za kujenga ‘camp site’ na uwekaji wa vipimo vya barabara ili kuanza kazi za uondoaji wa miundombinu ya taaasisi nyingine iliyomo ndani ya eneo la mradi.


Afisa Habari wa TARURA Bi. Catherine Sungura akitoa maelezo wakati wa semina katika semina ya kuwajengea uelewa waandishi wa habari wa mkoa wa Dar es Salaam kuhusu mipango na mikakati ya wakala huo.

Chapisha Maoni

0 Maoni