Tanzania inaviwango vya chini vya rushwa kwa nchi za EAC

 

Tanzania ni nchi ya pili kuwa na kiwango cha chini zaidi cha vitendo vya rushwa kati nchi kumi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirika la Kimataifa la Transparency.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Bw. Crispin Chalamila amebainisha hayo leo Machi 27, 2025 wakati akiwasilisha ripoti ya utendaji wa taasisi hiyo ya mwaka 2023/2024 kwa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Shirika Transparency kupitia kiashiria cha CPI ilitoa taarifa hiyo Februari 11, 2025 ambapo kwa mwaka 2024 Tanzania ilipata alama 41 juu ya 100 na kushika nafasi ya 82 kati ya nchi 180 zilizofanyiwa utafiti.

Pamoja na mambo mengine Bw. Chalamila amesema kwa mwaka 2023/24 TAKUKURU ilifanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi bilioni 30.1 kupitia operesheni mbalimbali za uchunguzi. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Bw. Crispin Chalamila kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Machi, 2025.

Chapisha Maoni

0 Maoni