Rais wa zamani wa Namibia Sam Nujoma afariki dunia

 

Rais wa kwanza wa Namibia huru, Sam Nujoma, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 95 katika mji mkuu wa Windhoek, kiongozi wa sasa wa nchi hiyo Nangolo Mbumba ametangaza.

Nujoma alikua rais mwaka 1990 na aliongoza nchi hadi 2005, baadatu ya nchi hiyo kupata uhuru.

Nujoma aliongoza vita vya muda mrefu vya kudai uhuru kutoka kwa Afrika Kusini mwaka 1990 baada ya kusaidia kupatikana kwa vuguvugu la ukombozi la Namibia lililojulikana kama South West Peoples' Organization (SWAPO) miaka ya 1960.

Nujoma alikuwa amelazwa hospitalini kwa muda wa wiki tatu zilizopita kutokana na ugonjwa ambao "hakuweza kupona", Rais Mbumba amesema katika taarifa yake akitangaza kifo hicho kwa "huzuni na masikitiko makubwa".

Chapisha Maoni

0 Maoni