Rais Samia aomboleza kifo cha Sam Nujoma wa Namibia

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa ameshtushwa na kuhuzunishwa na taarifa za kifo cha rais wa kwanza wa Namibia baaada ya uhuru na Baba wa Taifa hilo Sam Nujoma.

Katika salamu zake za pole, Rais Samia amesema kuwa Nujoma alikuwa ni mpigania uhuru, mwanamajumui wa Afrika na raifiki wa Tanzania ambapo aliishi wakati wa harakati wa kudai uhuru wa Namibia.

“Nujoma aliishi maisha ya si tu ya kujenga mustakabali wa taifa lake, bali alivivutia vizazi vya waafrika katika kusimamia dhana za uhuru, usawa na haki,” amesema Rais Samia kupitia akaunti yake ya Instagram.

Amemalizia kwa kusema kwamba, kwa niaba ya Serikali na watu wa Jumhuri ya Muungano wa Tanzania, anatoa salamu za pole kwa Rais wa Namibia Dk. Nangolo Mbumba, wananchi wa Namibia na Mke wa marehemu Kovambo Nujoma, watoto wake, familia yote, marafiki na komredi wa SWAPO.

Chapisha Maoni

0 Maoni