Rais Samia aitaka EAC na SADC kuhakikisha DRC inakuwa salama

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewahakikishi Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuwa Tanzania itaendelea kutoa ushirikiano katika kushughulikia mgogoro wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC).

Rais Dkt. Samia pia ametoa raia kwa Jumuiya hizo mbili kuchukua hatua ili kuhakikisha kuwa DRC ambayo ni mwanachama wa EAC na SADC, inakuwa salama na mgogoro unaondelea nchini humo unamalizika.

Rais Dkt. Samia ameyasema hao leo Februari 8, 2025 wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa pamoja wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa EAC na SADC uliofanyika katika Ikulu ya Dar es Salaam ili kujadili hali ya usalama Mashariki mwa DRC.

Amesema kuwa hali inayoshuhudiwa Mashariki mwa DRC haikubaliki na ipo haja ya kuchukua hatua za haraka kumaliza mgogoro huo unaoleta mateso kwa wananchi."Ninaimani kuwa mkutano huu utatoka na maazimio ambayo yatawezesha wananchi wa Mashariki mwa DRC kuishi kwa amani."

Kwa upande wake Rais wa Kenya ambaye pia ni Mwenyekiti wa EAC, Mhe. William Ruto amesema mgogoro unaoendelea Mashariki mwa DRC hautomalizwa kwa kutumia silaha bali kwa njia za kidiplomasia kupitia mazungumzo, kusikilizana na kushauriana.

Aidha, Rais Ruto amewataka wadau wote kushirikiana na Jumuiya za EAC na SADC katika kumaliza mgogoro huo ambao unaendelea kugharimu maisha ya wananchi wasio na hatia.

Chapisha Maoni

0 Maoni