Mloganzila kufanya upasuaji wa kuondoa minyama uzembe

 

Katika kuendelea kupambana na magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo magonjwa ya moyo, shinikizo  la juu la damu pamoja na kisukari, Hospitali ya Taifa Muhimbili  Mloganzila inaendelea na kambi maalum ya upasuaji rekebishi wa kupunguza mafuta katika sehemu mbalimbali za mwili kwa watu wenye uzito uliopitiliza ili kuwapunguzia athari ya kupata magonjwa hayo.

Daktari Bingwa wa Upasuaji MNH -Mloganzila, Dkt. Eric Muhumba amesema kambi hiyo inalenga kuwasaidia watu ambao walikuwa wakihangaika kupunguza uzito kwa njia mbalimbali bila mafanikio.

Ameongeza kuwa pamoja na kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza kambi hiyo pia inalenga kuwasaida baadhi ya watu ambao wamekuwa wakipata maumivu kutokana na baadhi ya viungo vyao vya mwili kuwa vikubwa kupita kiasi na kusababisha kupata maumivu ya mgongo.

Kambi hiyo itakayodumu kwa muda wa siku tano  kuanzia Februari 20 hadi 27, 2025 inafanyika kwa kushirikina  na Dkt. Shraddha Deshpande ambaye ni Bingwa wa Upasuaji Rekebishi kutoka nchini India. Mpaka sasa jumla ya watu sita wenye uzito uliopitiliza wamefanyiwa upasuaji huo.

Chapisha Maoni

0 Maoni