Wenje afichua njama za Lissu na Lema kutaka kumpindua Mbowe

 

Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Victoria, Ezekia Wenje amedai kuwa sababu iliyomfanya kutofautina na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu pamoja na Godbless Lema ni kukataa kuhusika na mapinduzi ya mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe wakati akiwa gerezani.

Bw. Wenje ameyasema hayo leo  Januari 16, 2025 akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku chache tu, tangu Lema azungumze kile alichodai kuwa Wenje hafai kuwa mwanachama wa Chadema kutokana na sifa zake.

Hata hivyo Wenje ambaye ni mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, yanakuja ikiwa ni siku chache kuelekea uchaguzi wa chama hicho huku minyukano baina yao ikiendelea kutoka kwa kambi za wagombe wa nafasi ya uenyekiti Mbowe na Lissu.

Chapisha Maoni

0 Maoni