Wahindu milioni kumi wajitakasa kwa kuoga mtoni

 

Zaidi ya watu milioni 10 wameshiriki tendo takatifu la kuoga kwa ajili ya kujitakasa, katika kusherehekea sherehe ya Wahindu ya Kumbh Mela, ambayo ni kusanyiko kubwa la binadamu katika mji wa India wa kaskazini wa Prayagraji.

Tukio hilo ambalo hufanyika kila baada ya miaka 12, limeanza jumatatu na kuendelea kwa wiki sita, ambapo waumini watajitakasa kwa kuoga kwenye mito inayochukuliwa kuwa ni mitakatifu ya Ganges, Yamuna na mythical Saraswati.

Wahindu wanaamini kuoga kwenye mito mitakatifu kunasafisha madhambi, kutakasa roho zao, na kuwakomboa katika mzunguko wa kuzaliwa na kufa, ili kufikia lengo la kupata ukombozi.

Mahujaji wapatao milioni 400 wanatarajiwa kuhudhuria sherehe hizo za siku 45, ambazo hupelekea eneo hilo kutokuwa na nafasi kutokana na umati mkubwa wa mamilioni ya watu wanaofika kujitakasa.

Mamlaka zimesema kwa siku ya Jumatatu watu milioni 10 wamejitakasa kwa kuoga, ambapo kesho jumanne watu watakaokuwa wamejitakasa kwa kuoga mtoni wanatarajiwa kuzidi milioni 20.




Chapisha Maoni

0 Maoni