Maria Sarungi kuongea leo baada ya kutekwa jana

 

Mwanaharakati na Mtetezi wa Haki za Binadamu Mtanzania Maria Sarungi Tshehai anatarajiwa kuongea leo na vyombo vya habari baada ya tukio lake la kutekwa jana Jijini Nairobi nchini Kenya.

Maria aliandika katika mtandao wake wa X jana baada ya kupatikana kuwa, yupo salama kwa sasa na kwamba ataongeza zaidi hapo kesho (leo).

“Asante sana kesho (leo) nitaongea vizuri, nipo salama, nimepambana nanyi mmepambana nipo salama asanteni wote Watanzania, Wakenya na Jumuiya za Kimataifa, kesho (leo) nitaongea .”

Taarifa za kutekwa kwa Maria ziliripotiwa na Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Amesty International nchini Kenya ambapo lilisema watekaji hao walifanya tukio hilo majira ya saa tisa na dakika kumi na tano alasiri wakiwa ni wanaume watatu wenye silaha wakiwa na gari jeusi aina ya Toyota Noah.

Chapisha Maoni

0 Maoni