Jeshi la Nigeria laua raia wake 16 kimakosa

 

Jeshi la Nigeria limewaua kimakosa raia 16 wa nchi hiyo katika shambulizi la anga baada ya kudhania kuwa ni kundi la wahalifu.

Wakazi wa eneo lilliloshambuliwa wameviambia vyombo vya habari walioshambuliwa ni kikundi cha kujilinda na raia wanaojitetea dhidi ya mashambulizi ya magenge yenye silaha yanayoteka nyara watu na kudai fidia.

Mashambulizi hayo ya anga yalikuwa yanalenga magenge ya wahalifu katika maeneo ya  Zurmi na Maradun, Gavana wa jimbo hilo Dauda Lawal amesema katika salamu zake za rambirambi.

Jeshi la Nigeria limekiri kufanya mashambulizi ya anga, ambayo yamewapa pigo kubwa magenge ya wahalifu wambayo yamemkuwa wakiwataabisha na kuwatia hofu wanavijiji katika eneo hilo.

Chapisha Maoni

0 Maoni